Journal of Kiswahili and Other African Languages
https://utafitionline.com/index.php/jkal
<p>The <strong>Journal of Kiswahili and Other African Languages</strong> is a high quality open-access, peer-reviewed and refereed multidisciplinary research journal, dedicated to serve the society by the global dissemination of information through an unparalleled commitment to quality, reliability, and innovation and research work. Journal of Kiswahili and Other African Languages welcomes and acknowledges high quality theoretical and empirical original research papers, case studies, review papers, literature reviews and conceptual framework from researchers, academicians, professional, practitioners and students from all over the world. Journal of Kiswahili and Other African Languages engages its noble efforts for the development and endeavours to give you the best.</p>UTAFITI FOUNDATIONen-USJournal of Kiswahili and Other African Languages2958-4914<p><a href="https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0/" rel="license"><img src="https://i.creativecommons.org/l/by-nc-sa/4.0/88x31.png" alt="Creative Commons License" /></a></p> <p>This work is licensed under a <a href="https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0/" rel="license">Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License</a>.</p>Mikakati ya Utetezi wa Mazingira katika Riwaya za Nakuruto na Bustani Ya Edeni
https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/1105
<p>Makala haya yanalenga kutathmini utetezi wa mazingira katika riwaya za <em>Nakuruto</em> (2009) ya Clara Momanyi na <em>Bustani ya Edeni</em> (2001) ya Emmanuel Mbogo. Kufuatia uharibifu wa mazingira kote ulimwenguni, utetezi wa mazingira umekuwa ukifanyika katika majukwaa mbalimbali yakiwemo makongamano ya kimataifa, mashirika ya uanaharakati na katika vyombo vya habari. Katika miaka ya hivi karibuni wanafasihi pia wameanza kutumia fasihi kama jukwaa la utetezi wa mazingira katika kazi zao za riwaya, tamthilia, hadithi fupi na ushairi. Jambo hili ndilo lililomvutia mtafiti kuchunguza namna suala la utetezi wa mazingira lilivyoshughulikiwa katika riwaya teule. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Uhakiki-Ikolojia kwa mujibu Glotfelty (1996). Muundo wa utafiti huu ni wa kimaelezo. Sampuli ya utafiti huu ni riwaya za <em>Nakuruto</em> (2009) na <em>Bustani ya Edeni </em>(2001) ambazo ziliteuliwa kimakusudi ili zichunguzwe. Matokeo ya utafiti huu yalionyesha kuwa mikakati mbalimbali kama vile dini, sheria, vyombo vya habari, mabango, nyimbo na maandamano imetumika kuyatetea mazingira. Makala haya yatawachochea wanaharakati wa mazingira katika kutumia majukwaa mbalimbali kuyatetea mazingira. Aidha, utafiti huu utapiga jeki juhudi za Wizara ya Mazingira katika kuhamasisha jamii kuhusu uharibifu dhidi ya mazingira.</p>Erick MainaLina AkakaRose Mavisi
Copyright (c) 2025
https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0
2025-06-242025-06-24321910.58721/jkal.v3i2.1105