Journal of Kiswahili and Other African Languages https://utafitionline.com/index.php/jkal <p>The <strong>Journal of Kiswahili and Other African Languages</strong> is a high quality open-access, peer-reviewed and refereed multidisciplinary research journal, dedicated to serve the society by the global dissemination of information through an unparalleled commitment to quality, reliability, and innovation and research work. Journal of Kiswahili and Other African Languages welcomes and acknowledges high quality theoretical and empirical original research papers, case studies, review papers, literature reviews and conceptual framework from researchers, academicians, professional, practitioners and students from all over the world. Journal of Kiswahili and Other African Languages engages its noble efforts for the development and endeavours to give you the best.</p> en-US <p><a href="https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0/" rel="license"><img src="https://i.creativecommons.org/l/by-nc-sa/4.0/88x31.png" alt="Creative Commons License" /></a></p> <p>This work is licensed under a <a href="https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0/" rel="license">Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License</a>.</p> Mon, 13 Jan 2025 00:00:00 +0000 OJS 3.3.0.16 http://blogs.law.harvard.edu/tech/rss 60 Uhifadhi wa Utamaduni kupitia Mchakato wa Tafsiri: Mifano ya Tafsiri ya Riwaya za Kaburi Bila Msalaba na Bwana Myombekere na Bibi Bugonoka, Ntulanalwo na Bulhawali https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/884 <p>Tafsiri ni mchakato wa kuhawilisha mawazo au ujumbe ulio katika lugha ya maandishi kutoka lugha chanzi kwenda katika lugha lengwa. Taaluma ya tafsiri inatumika kama nyenzo ya kueneza utamaduni, maarifa mapya, ujuzi, na uzoefu kutoka kwa jamii moja kwenda nyingine. Makala hii inakusudia kueleza jinsi utamaduni wa Kiafrika unadumishwa na kuhifadhiwa kupitia mchakato wa tafsiri. Makala iljikita katika uchanganuzi wa tafsiri ya <em>Kaburi Bila Msalaba </em>(1969) na<em> Bwana Myombekere na Bibi Bugonoka Ntulanalwo na Bulhawali</em> (1981). Makala hii ilipania kutoa maelezo jinsi tafsiri ya riwaya hizi ambazo ni hazina ya hifadhi ya utamaduni wa Kiafrika, inavyochangia na kuendeleza uhifadhi wa utamaduni kutoka lugha moja hadi nyingine. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya <em>Skopos </em>inayosisistiza lengo la tafsiri kuzingatiwa kabla ya zoezi la tafsiri kuanza. Data za utafiti huu zilikusanywa kwa kusoma na kuchambua matini chanzi <em>Kaburi Bila Msalaba </em>na<em> Bwana Myombekere na Bibi Bugonoka Ntulanalwo na Bulhawali </em>na matini lengwa, <em>Unmarked Grave </em>na<em> Mr. Myombekere and His Wife Bugonoka, Their son Ntulanalwo and Daughter Bulihwali</em>. Makala hii ililenga kuangazia vipengele vya kitamaduni vilivyohawilishwa kutoka utamaduni chanzi na kuingizwa kwa utamaduni lengwa na jinsi vinavyochangia uhifadhi wa utamaduni katika jamii mahususi. Mkabala wa kitaamuli ulitumika katika uwasilishaji wa data. Matokeo yalidhihirisha kwamba vipengele vya kitamaduni vimehawilishwa kutoka lugha moja kwenda nyingine hivyo basi, uhifadhi wa utamaduni umewezeshwa kupitia mchakato wa tafsiri.</p> Nyatichi Makini, Nathan Ogechi, Mosol Kandagor Copyright (c) 2025 https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0 https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/884 Wed, 15 Jan 2025 00:00:00 +0000 Athari ya Upokezi wa Matendo ya Utu kwa Binadamu: Mfano wa Riwaya za Said Ahmed Mohamed https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/936 <p>Ili pawepo na mahusiano mema kati ya binadamu, lazima pawepo na utu. Utu, hasa huhusishwa na binadamu. Hali kadhalika, huhusisha wema wowote unaomtendea mtu. Waandishi mbalimbali wa fasihi ya Kiswahili wamedhihirisha utu katika utunzi wao. Mtu anapopokea tendo la utu, huathirika kwa namna mbalimbali. Makala haya yanachunguza athari ya upokezi wa matendo ya utu kwa binadamu. Lengo kuu la makala ni kueleza binadamu anavyoathirika kwa njia mbalimbali kutokana na utu wa viumbe wa kiuhalisiajabu. Viumbe wa kiuhalisiajabu kama wanavyoitwa ni viumbe wenye sifa za kiajabuajabu. Ni viumbe tofauti na binadamu halisi na wenye nguvu fulani. Kutokana na nguvu hizo, huweza kufanya matendo mbalimbali.&nbsp; Makala iliongozwa na nadharia ya kiuhalisiajabu kama inavyofafanuliwa na Zamora na Wendy (1995). Muundo wa kimaelezo ulitumika huku eneo la utafiti likiwa fasihi ya Kiswahili, utanzu wa Riwaya. Sampuli ya kimakusudi ilitumika kuteua riwaya tatu za Said A. Mohamed hususan: <em>Babu Alipofufuka (2001),</em> <em>Dunia Yao (2006)</em> na <em>&nbsp;&nbsp;Nyuso za Mwanamke (</em>2010). Data ilikusanywa kutokana na kusoma riwaya hizo tatu zilizoteuliwa na kudondoa sehemu zilizolingana na malengo ya utafiti. Data ilidondolewa, ikanukuliwa, ikapangwa kisha kuchanganuliwa. Matokeo yalionyesha kuwa viumbe wa kiuhalisiajabu walidhihirisha utu kwa binadamu kwa namna mbalimbali na athari yake ikabainika. Utafiti huu unatoa mchango kwa walimu na wataalamu wa fasihi katika taaluma ya fasihi simulizi.</p> Peres Akello Obondo, Juliet Akinyi Jagero, Naomi Nzilani Musembi Copyright (c) 2025 https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0 https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/936 Tue, 18 Feb 2025 00:00:00 +0000 Matumizi ya Lugha katika Mandhari-Lugha ya Mji wa Njombe: Uchanganuzi wa Maandishi Katika Mabango ya Pikipiki https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/993 <p>Makala haya yamechunguza matumizi ya lugha katika mandhari-lugha ya mji wa Njombe, kwa kujikita katika maandishi yanayopatikana kwenye mabango ya pikipiki mjini humo. Lengo la utafiti lilikuwa ni kubainisha lugha inayotumika katika mabango ya pikipiki mjini Njombe. Aidha, utafiti ulilenga kuchanganua matumizi ya lugha katika muktadha wa jamii husika. Makala yaliongozwa na Nadharia ya Semiotiki ya Kijamii kama ilivyofafanuliwa na Michael Halliday (1978). Nadharia hii husisistiza kwamba lugha inaweza kuchunguzwa kikamilifu katika vipengele vya maana na dhima kwa kuihusisha na muktadha wa matumizi katika jamii husika. Data zilikusanywa kwa njia ya ushuhudiaji, upigaji picha na mahojiano huru. Data zilizokusanywa ziliwasilishwa kwa njia ya kimaelezo na takwimu. Matokeo ya utafiti yalibainisha kuwa 83.5% ya maandishi kwenye mabango ya pikipiki yalitumia lugha ya Kiswahili. Asilimia 16.5 ya maandishi iliyobaki ilijikita katika vikundi vitatu vya matumizi ya lugha, kila kikundi kikichukua 5.5%. Vikundi hivyo ni pamoja na maandishi yaliyochanganya Kiswahili na lugha ya kiasili, yale yaliyokuwa ya lugha ya kiasili pekee na yale ya lugha ya kigeni pekee. Aidha, ilibainika kuwa maandishi kwenye mabango ya pikipiki yalitumika kutekeza dhima mbalimbali kama vile kuhimiza umuhimu wa bidii na kazi, uadilifu, na uvumilivu. Isitoshe, baadhi ya maandishi yalitumika kujitambulisha na kujinasibisha, kuonyesha imani ya dini katika maisha ya binadamu pamoja na kubainisha uhuru alionao mtu katika kufanya maamuzi. Uelewa wa dhima hizi ulitokana na uelewa wa maana ya maandishi kwenye mabango hayo uliojikita katika muktadha wa jamii husika.</p> Leopard Jacob Mwalongo Copyright (c) 2025 https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0 https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/993 Sat, 12 Apr 2025 00:00:00 +0000 Sababu za Kupungua kwa Matumizi ya Majina ya Asili Nchini Tanzania: Mifano Kutoka Ginantuzu Lahaja ya Kisukuma https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/997 <p>Miaka ya hivi karibuni majina ya asili yamekuwa yakikabiliwa na changamoto ya kupotea&nbsp; kwa kasi isiyo kifani hasa kwa vijana nchini Tanzania. Makala hii imechunguza sababu za kupungua kwa matumizi ya majina ya asili katika koo za Ginantuzu, mojawapo ya lahaja za Kisukuma. Makala imeongozwa na baadhi ya maswali. Maswali hayo ni: Kwa nini majina ya asili yanapungua kila kukicha nchini Tanzania? Nini sababu za kupungua kwa matumizi ya majina ya asili hasa kwa vijana? Nini athari kwa jamii iwapo majina ya asili yakipotea? Data za makala hii zilikusanywa kwa mbinu ya ushuhudiaji, mahojiano, hojaji na mapitio ya nyaraka za maktabani, makavazi na mitandaoni. Makala ilitumia mkabala wa kitaamuli. Matokeo ya makala yameonesha kuwa, sababu za kupungua kwa matumizi ya majina ya asili katika koo za Ginantuzu ni mwingiliano wa ndoa katika familia, kuingia kwa dini ya Ukristo, kuporomoka kwa maadili kwa vijana, uhamiaji, kukosa umaarufu kwa majina ya asili, kasumba za ustaarabu kwa vijana, baadhi ya majina kupitwa na wakati, kukosa elimu kuhusu majina ya asili, na utandawazi. Aidha, makala pia inaonesha kuwa athari za kupotea kwa majina ya asili ni: kupoteza utambulisho wa jamii, kupoteza utamaduni, na kuhafifisha falsafa asilia za Ginantuzu zilizofumbatwa katika majina hayo. Makala inapendekeza kuwa wanajamii wanapaswa kupewe elimu kuhusu maana ya majina ya asili, pamoja na umuhimu wa kuyatumia. Hii itakuwa njia mwafaka ya kuhifadhi utamaduni, falsafa na historia ya jamii ya Ginantuzi kupitia majina ya asili.</p> Njana Masanja Copyright (c) 2025 https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0 https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/997 Tue, 15 Apr 2025 00:00:00 +0000 Kupotea kwa Maneno Chanzi katika Lahaja za Kiswahili: Uchunguzi Kifani wa Lahaja ya Kipemba https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/1006 <p>Tafiti mbalimbali zinaonesha kwamba, baadhi ya lahaja za Kiswahili zinaelekea kupoteza uasili wake kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za kijamii na kihistoria. Kupotea kwa maneno chanzi katika lahaja ni tatizo linalohitaji umakini wa haraka kwa sababu huenda kizazi kijacho kisiweze kuyatambua kabisa maneno hayo. Pamoja na ukweli huo, hakujawa na uchunguzi wa kina unaoonesha mifano kuntu ya maneno chanzi ambayo yanaonekana kupotea katika lahaja mbalimbali za Kiswahili ikiwamo lahaja ya Kipemba. Hivyo, makala hii inachunguza mifano ya maneno chanzi yanayoanza kupotea katika lahaja hiyo. Kwa hakika uchunguzi huu utasaidia kuyaweka bayana maneno hayo ili yabaki hai na yaendelee kutumiwa na watafiti pamoja na waandishi mbalimbali wa lugha ya Kiswahili na lahaja zake. Aidha, makala imechunguza sababu pamoja na athari za kupotea kwa maneno chanzi. Utafiti huu umeongozwa na Nadharia ya Umuundo iliyoasisiwa na De Saussure mwanzoni mwa karne ya 20. Data za makala hii zimekusanywa kupitia mbinu ya usomaji wa nyaraka, ushuhudiaji, usaili na hojaji. Makala imebaini kuwa kuna maneno chanzi mbalimbali ambayo yamepotea na mengine yanaendelea kupotea katika lahaja hiyo. Aidha, makala inatoa mchango mkubwa kwa taasisi za BAKITA na BAKIZA kwa kuwa zitaweza kuyatumia maneno hayo katika uundaji na usanifishaji wa istilahi za Kiswahili. Pia, watafiti na waandishi mbalimbali wa lahaja za Kiswahili wataweza kuyatumia maneno hayo katika tafiti zao. Makala imetoa mapendekezo ya kufanyika kwa uchunguzi zaidi wa maneno hayo katika lahaja nyingine mbalimbali za Kiswahili.</p> Sauda Uba Juma Copyright (c) 2025 https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0 https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/1006 Sun, 20 Apr 2025 00:00:00 +0000 Utata wa Baadhi ya Viambishi Tamati katika Vitenzi vya Kiswahili https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/1038 <p>Baadhi ya viambishi tamati katika vitenzi vya Kiswahili vimechanganuliwa na kuelezwa kwa namna zinazokinzana miongoni mwa wanaisimu mbalimbali. Makala hii inafafanua utata unaojitokeza katika suala hilo na kisha kupendekeza suluhisho muafaka. Makala hii ni matokeo ya utafiti wa mapitio ya machapisho pamoja tajiriba ya elimu ya sayansi ya lugha ya Kiswahili ya mwandishi akiwa na uzoefu wa kufundisha isimu ya lugha ya Kiswahili na Kiingereza chuoni kwa miaka zaidi ya kumi. Aidha, mwandishi anajenga hoja za kimantiki baada ya tafakari tunduizi ya masuala tatanishi huku hoja hizo zikishadadiwa kwa kupanua data husika. Upanuzi wa baadhi ya data ulisaidiwa na wadau wa Kiswahili katika makundi ya <em>WhatsApp ya Kiswahili </em>na isimu. Utata wa ufafanuzi na uchanganuzi unaooneshwa katika makala hii unahusu baadhi ya viambishi tamati ishilizi “<em>a, e, i </em>na <em>u</em>,’’ katika vitenzi vya Kiswahili. Halikadhalika, utata mwingine ni kuhusu viambishi tamati vilivyopata kuchanganuliwa au kubainishwa na wanaisimu waliotangulia. Baadhi ya wanaisimu wamechanganua kwa namna hii: “-<em>eni</em>/-<em>uni/-ini</em>” (mf. lim-<em>eni</em>/thubut-<em>uni/</em>safir<em>-ini</em>) huku wanaisimu wengine wakichanganua hivi: “-<em>ni</em>” (mf. lime-<em>ni/</em>thubutu<em>-ni/</em>safiri<em>-ni</em>). Makala hii imependekeza uchanganuzi na ufafanuzi mpya wa viambishi hivyo: <em>“-en-i</em>” (mf. lim-<em>en-i</em>), “-<em>un-i</em>” (mf. thubut-<em>un-i</em>) na “<em>in-i</em>” (mf. safir-<em>in-i</em>). Katika uchanganuzi huu mpya, viambishi -<em>en-, -un-,</em> na -<em>in- </em>vinarejelea dhana ya upamoja.</p> Issaya Lupogo Copyright (c) 2025 https://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/4.0 https://utafitionline.com/index.php/jkal/article/view/1038 Tue, 06 May 2025 00:00:00 +0000