Usawiri wa Ujumi katika Fasihi Simulizi: Uchambuzi wa Ngano za Wahehe
Keywords:
Sanaa, Fasihi, Fasihi Simulizi , Ngano , UjumiAbstract
Lengo la makala hii ni kujadili namna ujumi unavyosawiriwa katika fasihi simulizi, hususani ngano za Wahehe. Kusawiriwa kwa ujumi katika ngano za Wahehe kupitia vipengele vya ujumi kumeweka bayana uwiano wa vipengele hivyo na jamii husika. Aidha, athari zake kwa jamii husika zimebainishwa. Utafiti uliozaa makala hii ulitumia mbinu za kitaamuli. Data zilikusanywa kwa kutumia njia za uchambuzi matini na mahojiano. Ngano teule zilipatikana kwa kutumia sampuli lengwa. Utafiti na mjadala vimefanywa kwa kutumia Nadharia ya Ki-Marx iliyoasisiwa na Karl Marx na Fredrick Engels. Nadharia hii imekuwa faafu katika utafiti wa makala hii kwasababu inatumia mbinu za kipembuzi katika kuchanganua masuala ya kijamii na kiutamaduni. Matokeo yameonesha kwamba ujumi unaweza kusawirika katika ngano za Wahehe kupitia vipengele vyake, ambavyo ni ujumi katika mtu, asili, vitu, na sanaa. Aidha, vipengele hivyo vinaweka wazi idili za jamii husika zinazotokana na masuala mbalimbali yaliyopo kwenye jamii kama vile uongozi, malezi, ndoa, ufugaji, ulinzi, na kilimo.
Published
How to Cite
Issue
Section

This work is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License.
This work is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License.


